{ google_language = "en"; } { google_language = "en"; } KWA NINI UNALIA NA KUKATA TAMAA, jifunze na upate nguvu kwa aliyekuwa raisi wa marekani ~ MAKI INSPIRE

new

new job

http://go.oclasrv.com/afu.php?id=1313272

KWA NINI UNALIA NA KUKATA TAMAA, jifunze na upate nguvu kwa aliyekuwa raisi wa marekani

Abraham Lincoln hakukata tamaa
kamwe,kwanini wewe ukate tamaa?!
Alizaliwa katika umaskini, Lincoln alikuwa
mara nyingi anakabiliwa na kushindwa katika
maisha yake.
Alipoteza uchaguzi mara 8, mara 2 alishindwa
katika biashara na akakumbwa na ugonjwa
wa kuvunjika neva!
Angeweza kukata tamaa mara nyingi - lakini
hakufanya hivyo, na kwa sababu hakukata
tamaa,akawa mmoja wa marais wakubwa
katika historia ya Marekani!
Hii ni njia aliyopitia Lincoln kufika White
House:
1816 Familia yake ililazimishwa kutoka
nyumbani kwao.Ilibidi Lincoln afanye kazi ili
kuwasaidia.
1818 Mama yake alifariki.
1831 Alishindwa katika biashara.
1832 Aligombea ubunge-akashindwa
1832 Pia alipoteza kazi yake - alitaka kwenda
shule ya sheria lakini hakuchaguliwa.
1833 Alikopa fedha kutoka kwa rafiki yake ili
kuanzisha biashara lakini ilipofika mwisho wa
mwaka alikuwa amefilisika.Alitumia miaka 17
iliyofuata ya maisha yake kulipa deni hili!
1834 Aligombea ubunge tena - akashindwa.
1835 Aliingia kwenye uchumba ili afunge
ndoa,mchumba wake alifariki na moyo wake
ulivunjika sana.
1836 Alikumbwa na ugonjwa wa kuvunjika
neva na alikuwa kitandani kwa miezi sita.
1838 Aliwania kuwa msemaji wa bunge -
akashindwa.
1840 Aliwania kuwa mchaguzi - akashindwa.
1843 Aliwania Congress - akashindwa.
1846 Aliwania Congress tena - wakati huu
yeye alishinda - alikwenda Washington na
alifanya kazi nzuri.
1848 Aliwania kuchaguliwa tena Congress -
akashindwa.
1849 Aliwania kazi ya uafisa ardhi jimboni
kwake - akakataliwa.
1854 Aliwania kuwa Seneta - akashindwa.
1856 Aliwania uteuzi wa kuwa Makamu wa
Rais kupitia chama chake kitaifa - alipata
kura chini ya 100 na kushindwa.
1858 Aliwania kuwa Seneta tena -
akashindwa.
1860 ALICHAGULIWA KUWA RAISI WA 16 WA
MAREKANI!!

Yote yanawezekana pambana usikate tamaa

Share:

Related Posts:

No comments:

GET LATEST JOBS and VACANCIES UPDATES VIA EMAIL

Enter your name and e mail.

Get Latest Jobs Vacancies Alert Via Our Facebook Page

LATEST JOBS & VACANCIES